21 JUNI 2024
MP3•Episod hem
Manage episode 424785987 series 2027789
Innehåll tillhandahållet av UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations. Allt poddinnehåll inklusive avsnitt, grafik och podcastbeskrivningar laddas upp och tillhandahålls direkt av UN Global Communications (Digital Solutions Unit) and United Nations eller deras podcastplattformspartner. Om du tror att någon använder ditt upphovsrättsskyddade verk utan din tillåtelse kan du följa processen som beskrivs här https://sv.player.fm/legal.
Hii leo jaridani tunaangazia ziara ya Mwakilishi Maalum wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake huko Gaza, na masuala ya afya nchini Tanzania. Makala inatupeleka nchini Ethiopia na mashinani tunasalia nchini Tanzania, kulikoni? Baada ya ziara ya wiki moja huko Ukanda wa Gaza, Mashariki ya Kati, Maryse Guimond ambaye ni Mwakilishi Maalum wa shirika la Umoja wa Mataifa la masuala ya wanawake, UN Women katika eneo la Palestina linalokaliwa na Israeli,Israeli amesema kilicho alichoshuhudia hakina maelezo ya kutosha. Shirika la Umoja wa Mataifa la Afya ulimwenguni (WHO) nchini Tanzania kwa ufadhili wa Shirika la Maendeleo ya Kimataifa la Marekani (USAID), hivi karibuni limekabidhi kwa Wizara ya Afya nchini humo jengo maalumu kwa ajili ya kuwahudumia wanaohisiwa kuwa na magonjwa ya mlipuko ya kuambukiza wanapopita katika mpaka wa Mutukula unaounganisha Tanzania na Uganda kaskazini.Makala inatupeleka nchini Ethiopia ambako nchi hiyo kwasasa inatekeleza mpango wa kihistoria wa utoaji wa vitambulisho vya kitaifa unaojumuisha wakimbizi na wasaka hifadhi.Na mashinani tutakepeleka nchini Tanzania kusikia ujumbe wa watoto kuhusu elimu.Mwenyeji wako ni Assumpta Massoi, karibu!
…
continue reading
100 episoder